Skip to main content

Jinsi Ya Kulipwa YouTube

Bila shaka umeshasikia sana kuwa watu huingiza fedha kupitia channel zao za Youtube, lakini ni vipi fedha hizo huingia?
buy-adsense-safe-youtube-views
Je wale wenye views nyingi kama Diamond Platnumz ndio hupata fedha nyingi zaidi? Ni views ngapi unazohitaji ile kuingiza fedha kwenye YouTube? Hili ni swali la kawaida ambalo watu huuliza na jibu lake litategemea na nani umemuuliza.
Unaweza kuwa umesikia kuwa utaingiza dola moja kwa kila views 1,000 au $1,000 kwa views milioni moja. Wengine husema ni $5 kwa views 1000.
Mtandao wa videopower.org unadai kuwa tunauliza swali lisilo sahihi na kwamba tunatakiwa kuuliza ‘ni engagement gani inayohitajika ili kuingiza fedha kwenye Youtube?
Mtandao huo unasema huingizi fedha kwa kuzingatia kiasi cha views unachopata. Unatengeneza fedha kwa kuzingatia engagement ya watu kwenye tangazo.
Hapa engagement inamaanisha ni mtu kubofya na kuangalia tangazo kwa zaidi ya sekunde 30. Matangazo ya YouTube yanawezesha kwenye mfumo wa Adwords. Makampuni huchagua kuweka matangazo kwa njia mbili kuu; Cost Per Click (CPC) au Cost Per View (CPV).
Cost Per Click (CPC)
CPC ni pale kampuni inayotangaza inalipa fedha kwa kuzingatia clicks. Kwahiyo kama keyword fulani ikiwa na CPC ya $3 na mtu akaclick tangazo hilo, itaichaji kampuni hiyo $3. Maneno haya ya matangazo hutokea chini ya screen wakati unatazama video na huweza pia kutokea kama banner ya square upande wa kulia wa channel yako.
Cost Per View (CPV)
CPV ni pale kampuni inayotangaza inalipa fedha kwa kulingana na views. View kwa kampuni inayotangaza (advertiser) inamaanisha kuwa mtu anaangalia tangazo kwa walau sekunde 30 au nusu ya tangazo.
Mtu huyo anaweza kuclick tangazo hilo hata mara 50 lakini bado kampuni inayotangaza isitozwe kwasababu hailipi kwa click, wanalipa kwa view.
Kampuni inayotangaza hulipa tu pale mtu anapoclick au kuangalia tangazo kwa sekunde 30. Hii ndio maana huwezi kugeuza views za channel yako kuwa fedha. Kama video yako ikiangaliwa mara milioni 10 lakini hakuna mtu aliyeangalia au kuclick tangazo, huwezi kuingiza fedha yoyote.

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kutengeneza Channel Youtube.

Karibu tena ndugu msomaji na mtembeleaji wa blog yako pendwa ya Tanzania    ambayo inakupatia elimu itakayokusaidia kucopi na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayotokea kila leo. Katika makala ya leo tutaenda kuzungumzia namna ya kufungua channel ya youtube maarufu kama online TV . Makala hii itakwenda kukupa ujuzi wa namna ambayo utaweza kufungua channel ya youtube wewe mwenyewe, channel ambayo utaweza kuweka video zako na watu wengine wakapata kuziona. MAHITAJI 1 : G mail account 2: Kifaa chako cha kielectoniki (kama computer) 3: Internet connection HATUA ZA KUFUATA 1:Fungua mtandao wa youtube kwenye search engine yako mfano opera mini, mozila firefox. kisha tafuta (search) www.youtube.com kama hivi:- 2:Kisha baada ya hapo itafunguka na utatakiwa kuanza kwa ku  sign in  kama inavyoonekana hapa chini:- 3:Kisha baada ya hapo chagua  g mail  account yako ambayo uta  sign in  nayo ka...

Jinsi ya kuanzisha blog yako

Hapa ndio mahali husika katika kujifunza namna ya kuwa na blog yako na kuifanya iwe na mafanikio makubwa kama ambavyo wengine wamefanikiwa kupitia blog zao. Kuna namna mbali mbali za kuwa na blog ila leo hapa nitazungumzia mbili tu ambazo ni rahisi sana. Kumbuka kuwa kuwa na blog yako mwenyewe hakuna gharama yoyote zaidi ya muda wako na ubunifu wako. BLOGGER  Kupitia uwanja huo au platform hiyo inayomilikiwa na Google unaweza kuanzisha blog yako mwenyewe ambayo itabebwa na jina ulipendalo wewe mfano:- http:// blogyako .blogspot.com, hapo ambapo nimekoleza kwa maandishi ya rangi nyekundu ndipo ambapo utaweka jina la blog yako. Utaratibu mzima utaupata wakati ukiwa unaisajiri blog yako Bofya hapa ili kutengeneza blog yako  Create a new Blog   WORDPRESS  Hapa pia utaratibu ni kama hapo mwanzo ila hizi ni nyanja (Platforms) tofauti na zinatofautiana vikolombwezo (features)  vya uboreshaji wa blogs. Hapa ukianzisha blog yako itabebwa na uwanja au platform...

Utapata kwa siku 60000 kupitia blog!!!

Ndio inawezekana na kwa namna rahisi au kwa namna ngumu kutokana na jinsi ambavyo umejipanga katika blog yako na njia ambazo unazitumia kutengeneza hela kwa blogu.   Kuna njia nyingi sana za kutengeneza hela kwa kutumia blogu kwa uchache ni  Google Adsense, Kuuza vitu, Watu kulipia kuona blog yako, Matangazo  n.k Nimeaainisha kwa ufupi namna ya kupata hela ila endelea kutembelea blog hii kwani nitakuwa nikielezea moja baada ya lingine kwa undani zaidi. Lakini yote kwa ujumla yanategemea mambo makubwa ya yafuatayo. IDADI /Traffic  – Hapa idadi inayozungumziwa ni ya watu wanaotembelea blogu yako kwa siku. Kama blog yako ina watembelaaji wengi kwa siku kiasi cha kufikia 1000 basi ni wazi kuwa utakua katika nafasi nzuri ya kutengeza hela katika blog yako. Kwani IDADI/Traffic kubwa ya watembeleaje itavutia watangazaji katika kutangaza kwa blog yako. MADA /CONTENT  – Hapo jambo la kuzingatia ni kuwa blogu yako yajihusisha na nini zaidi...