Skip to main content

Jinsi ya kunufaika na blog au tovuti yako


Naam ni wengi sana wamekuwa wakianzisha blog au tovuti na kuishia njiani bila kuona mafanikio. Hapa nitazungumzia mambo makuu ambayo kama ukizingatia basi utafanikiwa katika blogu yako au tovuti. Kuna mambo ya kuzingatia kabla ya kuamua kuanzisha blogu au tovuti yako.



  • MADA /TOPIC  ni swala la muhimu sana kuzingatia kabla hujaanzisha blogu au tovuti yako. Wengi  wemeshindwa kutoka na kutokujipanga katika swala hili. Kama unataka kuwa na blog kwa ajili ya habari basi uwe umejipanga vizuri katika kupata habari mpya na sio kunakili kutoka katika blog zingine za habari. Wadau wengi wanaanzisha blogu ila hawaoni mafanikio kwa vile hawana kitu cha kuvuta wadau katika blogu zao.
·         8020fashions ni moja ya blog ambayo imefanikiwa sana hapa Tanzania, mwanadada huyo yeye amejikita katika mambo ya wanawake. Hachanganyi mambo.

·         Issamichuzi  pia ni blog yenye mafanikio makubwa sana kwa vile yeye ni mwanahabari na blog yake ni ya habari. Wengi mnakosea kwa vile mnaanzisha blog za habari ila hamtafuti habari bali mnanakili kutoka kwake
  • PATA MUDA wa kutosha katika kushughulia blogu yako ili kuweza kuyaona mafanikio. Wengi wanakata tamaa mapema kwa vile hutaka mafanikio ya haraka sana katika blogu na tovuti.
  • JITANGAZE , kuna namna nyingi za kuweza kuitangaza blogu yako na kufanya ifahamike na wengi. Unaweza fanya link exchange kutoka kwa watu wengine wenye blogs. Ni kuwa unaweka link zao kwako na wewe unawaomba waweke link yako kwako.  Vile vile waweza inadi blog yako kwa njia ya radio, google adwords. Mada hii ni ndefu sana ya namna ya kuinadi blog yako. Endelea kutembelea blog hii nami nitakuwa naleta mada mbali mbali za kukusaidia katika kuinadi blog yako.
  • MATANGAZO, kama utaweza kuvutia watangazaji katika blog yako basi utakua umefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Ila hili litawezekana kama ukizingatia mambo ambayo nimeyazungumzia hapo juu.
Nisikuchoshe kwa leo. Hadi wakati mwingine tena. Tafadhali kwa lolote lile kuhusu blogu na tovuti wasiliana nami kupitia barua pepe hapa masakafrances6@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kutengeneza Channel Youtube.

Karibu tena ndugu msomaji na mtembeleaji wa blog yako pendwa ya Tanzania    ambayo inakupatia elimu itakayokusaidia kucopi na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayotokea kila leo. Katika makala ya leo tutaenda kuzungumzia namna ya kufungua channel ya youtube maarufu kama online TV . Makala hii itakwenda kukupa ujuzi wa namna ambayo utaweza kufungua channel ya youtube wewe mwenyewe, channel ambayo utaweza kuweka video zako na watu wengine wakapata kuziona. MAHITAJI 1 : G mail account 2: Kifaa chako cha kielectoniki (kama computer) 3: Internet connection HATUA ZA KUFUATA 1:Fungua mtandao wa youtube kwenye search engine yako mfano opera mini, mozila firefox. kisha tafuta (search) www.youtube.com kama hivi:- 2:Kisha baada ya hapo itafunguka na utatakiwa kuanza kwa ku  sign in  kama inavyoonekana hapa chini:- 3:Kisha baada ya hapo chagua  g mail  account yako ambayo uta  sign in  nayo ka...

Jinsi ya kuanzisha blog yako

Hapa ndio mahali husika katika kujifunza namna ya kuwa na blog yako na kuifanya iwe na mafanikio makubwa kama ambavyo wengine wamefanikiwa kupitia blog zao. Kuna namna mbali mbali za kuwa na blog ila leo hapa nitazungumzia mbili tu ambazo ni rahisi sana. Kumbuka kuwa kuwa na blog yako mwenyewe hakuna gharama yoyote zaidi ya muda wako na ubunifu wako. BLOGGER  Kupitia uwanja huo au platform hiyo inayomilikiwa na Google unaweza kuanzisha blog yako mwenyewe ambayo itabebwa na jina ulipendalo wewe mfano:- http:// blogyako .blogspot.com, hapo ambapo nimekoleza kwa maandishi ya rangi nyekundu ndipo ambapo utaweka jina la blog yako. Utaratibu mzima utaupata wakati ukiwa unaisajiri blog yako Bofya hapa ili kutengeneza blog yako  Create a new Blog   WORDPRESS  Hapa pia utaratibu ni kama hapo mwanzo ila hizi ni nyanja (Platforms) tofauti na zinatofautiana vikolombwezo (features)  vya uboreshaji wa blogs. Hapa ukianzisha blog yako itabebwa na uwanja au platform...